Business

Lishe Bora Yaongeza Uzalishaji wa Maziwa Kilifi, Lakini Soko Labanwa

Published

on

Wafugaji ng’ombe za maziwa kaunti ya Kilifi wamesema kiwango cha maziwa wanachopata kwa sasa kimeongezeka msimu huu wa mvua ikilinganishwa na msimu wa kiangazi.

Kulingana ma mmoja wa wafugaji hao katika kijiji cha Bodoi Wadi ya Junju kaunti ya Kilifi Leonard Zuma,kwa sasa wanapata maziwa mengi ikilinganishwa na miezi ya nyuma kutokana na upatikanaji wa urahisi wa nyasi.

Akizungumza na meza yetu ya Biashara ,Zuma amesema kwamba kwa sasa anatoa lita 20 kwa kila ng’ombe kinyume na hapo awali.

“ kwa sasa nyasi zinapatika kwa wingi ikilinganishwa na hapo awali ambapo tulikuwa tunanunua nyasi jambo ambalo limefanya kiwango cha maziwa kuongezeka.”

Hata hivyo Zuma amedokeza kuwa hakuna soko la kupeleka maziwa yao hali ambayo inapelekea kwamba kwa sasa wanapitia changamoto ya uhaba wa wateja katika soko la maziwa kutokana na hali ya uchumi ilivyo kwa sasa huku akilalamika ughali wa daktari wa ng’ombe.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version