Sports

Twende Kasarani Tushabikie Stars- Asema Waziri Mvurya

Published

on

Waziri wa michezo Salim Mvurya ametangaza  kwamba matayarisho ya michuano ya CHAN yamekamilika na vijana wa nyumbani wako tayari kuakilisha Taifa.
Kenya itatumia viwanja vya  Kasarani, na Nyayo,  huku viwanja vya Polisi SACCO, Kasarani Annex na  Ulinzi sports Complex, vikitumika Kwa mazoezi ya timu zote zinazoshiriki michuanobuii.
Akizungumza mjini Kilifi, Waziri Mvurya aliwahakikishia Wakenya burudani huku akiwaalika kujitokeza Kwa wingi kushabikia timu ya Taifa Harambee Stats.
Ukarabati wa Viwanja hivi viwili umekamilika hivi majuzi na kukabidhiwa rasmi Kwa Kamati andalizi ya michuano hiyo kwenye hafla iliyohudhuriwa na Waziri wa Usalama Kipichunba Murkomen na Waziri Mvurya.
 Timu ya Taifa Harambee stars itafungua dimba hilo ikiwa katika Kundi A pamoja na DR Congo, Morocco, Zambia na Angola. Kundi hili kimetajwa kuwa gumu zaidi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version