National News

KUPPET Yataka Walimu Kupewa Usalama

Published

on

Naibu katibu wa Chama cha Walimu wa shule za upili na vyuo vya kadri nchini KUPPET kaunti ya Kilifi Opollo Zacharia Kopolo ametoa wito kwa serikali kuu kuhakikisha walimu ambao wanafunza katika maeneo ambayo hayana usalama wa kutosha kuimarishiwa usalama.

Kopolo amesema hatua hiyo itachangia kuzikabili changamoto mbalimbali ambazo walimu hao wamekuwa wakipitia na kuchangia matokeo duni ya elimu.

Kopolo amesema ni jukumu la serikali kuu kuhakikisha walimu wanafanya kazi katika mazingira bora kwani imekuwa vigumu kwao kuwafunza wanafunzi ipasavyo kama wanafunzi wengine nchini.

Vilevile, Kopolo amesema kuna baadhi ya walimu ambao wamekuwa wakikataa kufunza katika maeneo hayo ambayo yanakabiliwa na utovu wa usalama wakihofia usalama wao hali ambayo inachangia kwa wanafunzi kuandikisha matokeo duni.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version