Sports

Kocha Wa Starlets Odemba ajiuzulu

Published

on

Mkufunzi wa timu ya taifa soka akina dada Harambee Starlets Beldine Odemba ametangaza kujizulu wadhifa wake kama kocha mkuu wa kikosi hicho baada ya kichapo cha magoli 5-1 na Morocco mechi ya kirafiki.

Kwa mujibu wa mwalimu huyo kilichomfanya kuondoka katika kambi ya timu hiyo ni kukosa ungwaji mkono katika kazi yake ya kunoa starlets akiondoka siku chache tuu kabla ya kungoa nanga kwa taji Cecafa nchini Tanzania Juni 12.

Mkufunzi huyo ambaye ameshinda ligi ya akina dada na kilabu ya Kenya Bullets amedokeza kwamba ni swala ambalo ameliwazia kwa muda na kwa sasa anaelekeza nguvu zote kwa kikosi hicho taji la Cecafa baina ya vilabu.

Ripoti zinaarifu kwamba kocha wa Kibera Soccer Women David Vijago atatangazwa kocha mpya wa Starlets akisaidiana na Alex Alumira ambaye amewahi kuwa kocha wa timu hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version