Sports

Kocha Nyamunyamu Tulikosa Taji Kwani Wachezaji Waliondoka

Published

on

Kocha wa kilabu ya akina dada Vihiga Queens ya Magharibi Bonface Nyamunyamu amesema kwamba kwa sasa wanaangazia kupata taji la akina dada FKF Cup baada ya ligi ya akina dada KWPL kuwaponyoka msimu huu.

Akizungumza na Kipenga cha COCO FM mwalimu huyo amekiri ilikua vigumu wao kumaliza kileleni kutokana na mabadiliko makubwa kikosini msimu uliopita.

“Ligi ilikua ngumu kwetu kushinda msimu huu kwa sababu tulipoteza wachezaji wengi mahiri ,tulipoteza kipa wetu namba moja ,tukapoteza pia mabeki wetu tegemeo wawili kwa wapinzani wetu pia tukapoteza mshambulizi wetu mahiri haya yote ukiweka kwa pamoja yalitatiza kikosi changu kwani ilibidi tuanze upya na wachezaji wengine.”

Hata hivyo mwalimu huyo sasa anaamini na kikosi walichonacho watakuwa vizuri msimu ujao kupigania ubingwa wa ligi ambayo imewaponyoka tangu mwaka 2021.

Kilabu hiyo ilimaliza nafasi ya 4 msimu uliokamilika na alama 38 ligi iliotwaliwa na kilabu Kenya Police Bullets.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version