Sports

Kikosi Cha Raga Simbas Yashinda Tena

Published

on

Kikosi cha Raga wachezaji 15 kila upande Simbas imepata ushindi wake wa pili katika mechi za kujipima nguvu kabila ya kombe la bara Afrika baadaye mwakani.

Simbas waliwatandika Super Babarians alama 27-22 mechi iliopigwa mjini Lumpopo Afrika Kusini.

Vijana hao wa kocha Jerome Parwater walikua wametoka sare mechi mbili 17-17 dhidi ya SWD Eagles na vilevile kupteza mechi mbili dhidi ya Chipukizi wa Afrika Kusini Blitz Bocks na Sanlam Bolam.

Timu hiyo imesalia na mechi moja ya kirafiki dhidi ya Limpompo kabila ya mashindano ya kombe la Bara Afrika mjini Kampala Uganda mwezi Julai mechi hizo zikitumika pia kama mechi za kombe la dunia nchini Australia mwaka 2027.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version