Sports

Kevin De Bruyne Atua Napoli

Published

on

Ni rasmi kilabu ya Napoli imetangaza kupata sahihi ya kiungo wa zamani wa Manchester City Kevin De Bruyne raia wa Ubelgiji.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 amewaga wino kwenye karatasi kandarasi ya miaka miwili na mabingwa hao wa Serie A.

Kupitia kwenye tuvuti ya kilabu hiyo Rais Aureli De Laurenttis ameweza kuthibitisha kuwasili kwa nyota huyo ambaye aliwika sana ligi kuu uingereza akishinda kila kitu na Mancity kwa kumwambia ‘KARIBU NAPLES’.

Kiungo huyo mbunifu alitangaza kuondoka City baada ya kuwajibikia kilabu hiyo kwa muda miaka minane akishinda mataji sita ligi ya EPL ,Moja kilabu bingwa ulaya,manne ya FA na mataji mengine.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version