News
Kadinali Farrell: Papa Francis Atazikwa Jumamosi Aprili 26
Uongozi wa Kanisa Katoliki mjini Vatican umetangaza kwamba Papa Francis atazikwa siku ya Jumamosi Aprili 26 katika Kanisa kuu la mtakatifu Bikiri Maria mkuu kuanzia mwendo wa saa nne asubuhi kwa kuambatana na Ibada ya Misa.
Kulingana na Kadinali Kevin Farrell, Camerlengo wa baraza la kitume la Kanisa Katoliki, uamuzi huo umeafikiwa kufuatia mkutano wa makadinali wote waliowasili Vatican kwa mipingo na maadilinzi ya mazishi kabla ya waumini wa Kanisa Katoliki kuruhusiwa kuutazama mwili wa Papa.
Kadinali Farrell amesema kwa kuzingatia kanuni na desturi za Kanisa Katoliki baada ya Papa kuaga dunia, Kanisa limefunga makaazi ya Papa kwa kitambaa chekundu kuashiria kwamba Papa amefariki na mwili wake umewekwa ndani ya jeneza katika Kanisa la Casa Santa Marta mjini Vatican huku maombi maalum yakiendelea.
Kulingana na desturi za Kanisa Katoliki baada ya mazishi makadinali watakusanyika pamoja katika chumba maalamu yaani Conclave ili kuanza mchakato wa kumchagua Papa mpya katika kipindi cha siku 15 hadi 20 na mchakato huo umepangwa kuanza rasmi mwezi Mei tarehe 5.
Pete ya Papa Francis, pia huvunjwa na kuharibiwa ishara ya ukomo wa maisha yake ya Papa.
Itakumbukwa kwamba Papa Francis aliaga dunia mnamo siku ya Jumatatu Aprili 21 mwendo wa saa moja na nusu asubuhi baada ya kuugua dunia akiwa na umri wa miaka 88.