News
Kadinali Farrell: Papa Francis Atazikwa Jumamosi Aprili 26

Uongozi wa Kanisa Katoliki mjini Vatican umetangaza kwamba Papa Francis atazikwa siku ya Jumamosi Aprili 26 katika Kanisa kuu la mtakatifu Bikiri Maria mkuu kuanzia mwendo wa saa nne asubuhi kwa kuambatana na Ibada ya Misa.
Kulingana na Kadinali Kevin Farrell, Camerlengo wa baraza la kitume la Kanisa Katoliki, uamuzi huo umeafikiwa kufuatia mkutano wa makadinali wote waliowasili Vatican kwa mipingo na maadilinzi ya mazishi kabla ya waumini wa Kanisa Katoliki kuruhusiwa kuutazama mwili wa Papa.
Kadinali Farrell amesema kwa kuzingatia kanuni na desturi za Kanisa Katoliki baada ya Papa kuaga dunia, Kanisa limefunga makaazi ya Papa kwa kitambaa chekundu kuashiria kwamba Papa amefariki na mwili wake umewekwa ndani ya jeneza katika Kanisa la Casa Santa Marta mjini Vatican huku maombi maalum yakiendelea.
Kulingana na desturi za Kanisa Katoliki baada ya mazishi makadinali watakusanyika pamoja katika chumba maalamu yaani Conclave ili kuanza mchakato wa kumchagua Papa mpya katika kipindi cha siku 15 hadi 20 na mchakato huo umepangwa kuanza rasmi mwezi Mei tarehe 5.
Pete ya Papa Francis, pia huvunjwa na kuharibiwa ishara ya ukomo wa maisha yake ya Papa.
Itakumbukwa kwamba Papa Francis aliaga dunia mnamo siku ya Jumatatu Aprili 21 mwendo wa saa moja na nusu asubuhi baada ya kuugua dunia akiwa na umri wa miaka 88.
News
Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.
Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.
Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.
Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro
Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.
Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.
Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.
Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.
‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.
Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.
Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.
Taarifa ya Janet Mumbi