Sports

Harambee Stars Yavuna Ushindi Dhidi Ya Chad

Published

on

Timu ya taifa ya soka Harambee Stars imevuna ushindi wa kwanza chini ya kocha Benni McCarthy baada ya kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Chad Ugani Stade De Marrekesh Morocco.

Mshambulizi wa kilabu ya Talanta fc Emmanuel Osoro aliwatanguliza vijana wa nyumbani dakika ya 18 kabila ya mshmabulizi wa Bandari Fc David Sakwa kufunga goli la pili dakika ya 45.

Hata hivyo Chad inayoshikilia nafasi ya 177 kote ulimwenguni ilerejea kwa kishindo kipindi cha pili wakijipatia goli la kufutia machozi dakika ya 60.

Kocha wa Stars anamini angali anajenga kikosi ambacho kitakua bora zaidi katika miaka za mbeleni huku akiahidi vijana wa nyumbani wataleta furaha kwa Wakenya.

“Ushindi ni Muhimu lakini bado najitahidi kuwajua vijana wangu kwa muda mrefu mashabiki wawe na utulivu kwani Stars itafurahisha hivi karibuni.”

Hii ilikua ni ushindi wa kwanza kwa kocha huyo tangu achukuwe mikoba kutoka kwa kocha mkuu Engine Firat alionyeshwa mlango kutokana na msururu wa matokeo duni.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version