News
Alshabab yauwa KDF watatu Lamu
Wanajeshi watatu wa Kenya wameuawa, huku wengine saba wakiwachwa na majeraha mabaya mwilini, baada ya gari walimokuwa wakisafiria kukanyanga kilipuzi eneo la Badaah, kaunti ya Lamu.
Naibu kamishna kaunti ya Lamu Mashariki George Kubai alisema wanajeshi hao walikuwa wakiwapeleka wenzao eneo la Sankuri kutoka Kiunga wakiwa kwenye gari jingine wakati gari lao lilipokanyaga kilipuzi hicho kilichozikwa ardhini.
Waliojeruhiwa wanapokea matibabu katika hospitali ya Kiunga huku vyombo vya usalama vikianzisha oparesheni kuwasaka magaidi waliotega kilipuzi hicho.
Kaunti ya Lamu imekuwa ikishuhudia mashambulizi ya kigaidi yanayotekelezwa na mgaidi wa alshabab kutoka taifa jirani la Somalia.
Taarifa ya Joseph Jira