News
Washukiwa wa uhalifu wakamatwa maeneo ya Likoni kaunti ya Mombasa
Mafisa kutoka kituo cha polisi cha Vijiweni eneo la Likoni kaunti ya Mombasa, usiku wa kuamkia leo wamewakamata wanaume watatu wanaoshukiwa kuwa wahalifu katika maeneo ya Likoni na sehemu za Kaunti ya Kwale.
Kulingana na ripoti za polisi, watuhumiwa hao, Abubakar Juma Koba mwenye umri wa miaka 17, Ali Bakari mwenye umri wa miaka 17 na Mohamed Ruwa mwenye umri wa miaka 18 ni wanachama wa kundi la vijana wanaotumia mapanga, ambao wanashutumiwa kwa kuwahangaisha wakazi katika maeneo ya Mwaweche Magulani na Dongo Kundu.
Watuhumiwa walikamatwa wakati wa doria ya usiku kufuatia taarifa za kijasusi.
Wengine watano walifanikiwa kutoroka.