News

Wazee wa Kaya Wanataka Bandari ya Mombasa Kuwafaidi Wenyeji

Published

on

Muungano wa Wazee wa Kaya eneo la Pwani unaitaka serikali ya kitaifa kubuni mikakati ya kuhakikisha bandari ya Mombasa inawafaidi wenyeji wa Pwani hasa katika suala la utoaji ajira.

Muungano huo umesema bandari ya Mombasa inafaa kuendeshwa na watu wanaowajibika kikamilifu ili kuchangia pato la taifa na kuimarisha uchumi wa Pwani.

Mshirikishi wa Muungano huo wa Wazee wa Kaya kanda ya Pwani Tsuma Nzai Kombe, ameitaka serikali kutohusisha utendakazi wa bandari ya Mombasa na masuala ya kisiasa na badala yake kuangazia jinsi wananchi watakavyonufaika na taasisi hiyo.

Upande wake Mwenyekiti wa Wazee hao wa Kaya Mwaringa Juma amemtaka rais Ruto kukutana na wazee hao ili kuzungumzia suala la ajira kwa vijana wa Pwani.

Hata hivyo Msemaji wa Muungano wa Wazee wa Kaya na ambaye pia ni kiongozi wa Vijana Nguma Charo ameitaka serikali kuangazia suala tata la ardhi katika eneo la Pwani sawa na changamoto ya ajira kwa vijana.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version