News

Walimu 294 wa shule za chekechea wamepandishwa vyeo Taita Taveta

Published

on

Jumla ya walimu 294 wa shule za chekechea kaunti ya Taita Taveta wamepandishwa vyeo kulingana na kiwango chao cha masomo yao.

Akiwahutubia walimu hao gavana wa kaunti ya Taita Taveta Andrew Mwadime alisema hatua hiyo inalenga kuboresha utendakazi sawa na kuwatia motisha baada ya juhudi zao kukosa kutambuliwa kwa mda mrefu.

Hata hivyo Mwadime aliwataka walimu hao kuwajibika zaidi katika maeneo yao ya kazi, akitaja sekta ya elimu kuwa nguzo muhimu katika ujenzi wa jamii bora na iliyo na maadili.

“Mlikuwa mnafanya kazi kwa muda mrefu, mlikuwa mnafundisha, mwalipwa elfu tatu, saa ingine mwaenda bila mshahara.Hamna aliyemtambua hapo awali’’, alisema Mwadime.

Ni Kauli iliungwa mkono na naibu gavana wa kaunti hiyo Christine Kilalo ambaye aliwahimiza walimu hao kuwafunza watoto ipasavyo ili viwango vya elimu kwenye kaunti hiyo viweze kuimarika hata zaidi.

Walimu waliopandishwa cheo ni kati ya walimu 697 wanaofundisha katika shule mbalimbali za chekechea kaunti ya Taita Taveta.

Taarifa ya Janet Mumbi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version