News
Kalonzo ataka serikali kufafanua kuhusu uwepo wa maafisa wa Jubaland nchini.
Kinara wa chama cha Wiper Kalonzo Msyoka ameitaka serikali ya rais William Ruto kutoa ufafanuzi kuhusu uwepo wa maafisa kutoka Jubaland hapa nchini.
Kalonzo alisema hatua hiyo inazua maswali mazito kuhusu usalama wa taifa.
Kinara huyo aliongeza kuwa hali ya usalama nchini imeendelea kutatizika huku raia wa maeneo ya mipakani kama Mandera wakiishi kwa hofu ya kuhatarisha maisha yao.
Alisema kitendo cha maafisa wa usalama kutoka taifa jirani kuwepo hapa nchini bila maelezo ya wazi kinaweza kuchochea mzozo wa kiusalama na kuathiri utulivu wa kitaifa.
Viongozi wa kisiasa na wananchi walieleza wasiwasi wao kuhusu athari za hali hiyo wakitaka serikali kutoa maelezo ya kina na kuchukua hatua za haraka kuhakikisha mipaka ya nchi inalindwa ipasavyo.
Taarifa ya Joseph Jira.