News

Wachungaji 85 Adu, Kilifi wapokea mafunzo ya kukabili itikadi kali

Published

on

Jumla ya wachungaji 85 kutoka wadi ya Adu eneo bunge la Magarini kaunti ya kilifi wanaendelea kupokea mafunzo ya kidini kuhusu sheria zinazoambatana na utoaji wa mafunzo ya dini katika makanisa.

Wakiongozwa na Johnson Kaingu mchungaji wa kanisa la PGM Ramada, wachungaji hao walisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia pakubwa kudhibiti makanisa yanayoendeleza mafunzo ya imani potofu.

Wachungaji hao aidha walipongeza mpango huo wakisema utatoa mwelekeo wa jinsi wachungaji wanavyostahili kuhudumu pasi na kupotosha waumini.

“Tuliposikia habari zile za Shakahola tuliona si vizuri tubaki hivyo ila tupate mafundisho maalum kama wachungaji, ili tuweze kudhibiti makanisa yetu yasiangukie mtego ule wa Shakahola. Ufahamu huu ambao umeletwa huku kwetu Adu umetufanya sisi tutakuwa hata tukisimama tutakuwa hata tukisimama tunajua tunafundisha nini ili watu wa Mungu tujue tutawaelekeza katika njia ambayo inafaa”,walisema wachungaji.

Kwa upande wake Elizabeth Dama mmoja wa wachungaji hao ameupongeza mpango huo akisema utawasaidia kutoa mafunzo ya kweli kwa waumini.

“Tuko wachungaji 85 kupitia Christian Pass ambao wametushika mkono ndio wanatufadhili tufundishwe ndio wanalipa walimu”,alisema mchungaji Dama.

Mafunzo hayo yanayofadhiliwa na shirika la Christian Pass yanajiri baada ya kushuhudiwa kwa idadi kubwa ya maafa ya watu katika msitu wa Shakahola sawa na eneo la Kwa Binzaro kupitia mafunzo ya dini potofu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version