Connect with us

News

Wachungaji 85 Adu, Kilifi wapokea mafunzo ya kukabili itikadi kali

Published

on

Jumla ya wachungaji 85 kutoka wadi ya Adu eneo bunge la Magarini kaunti ya kilifi wanaendelea kupokea mafunzo ya kidini kuhusu sheria zinazoambatana na utoaji wa mafunzo ya dini katika makanisa.

Wakiongozwa na Johnson Kaingu mchungaji wa kanisa la PGM Ramada, wachungaji hao walisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia pakubwa kudhibiti makanisa yanayoendeleza mafunzo ya imani potofu.

Wachungaji hao aidha walipongeza mpango huo wakisema utatoa mwelekeo wa jinsi wachungaji wanavyostahili kuhudumu pasi na kupotosha waumini.

“Tuliposikia habari zile za Shakahola tuliona si vizuri tubaki hivyo ila tupate mafundisho maalum kama wachungaji, ili tuweze kudhibiti makanisa yetu yasiangukie mtego ule wa Shakahola. Ufahamu huu ambao umeletwa huku kwetu Adu umetufanya sisi tutakuwa hata tukisimama tutakuwa hata tukisimama tunajua tunafundisha nini ili watu wa Mungu tujue tutawaelekeza katika njia ambayo inafaa”,walisema wachungaji.

Kwa upande wake Elizabeth Dama mmoja wa wachungaji hao ameupongeza mpango huo akisema utawasaidia kutoa mafunzo ya kweli kwa waumini.

“Tuko wachungaji 85 kupitia Christian Pass ambao wametushika mkono ndio wanatufadhili tufundishwe ndio wanalipa walimu”,alisema mchungaji Dama.

Mafunzo hayo yanayofadhiliwa na shirika la Christian Pass yanajiri baada ya kushuhudiwa kwa idadi kubwa ya maafa ya watu katika msitu wa Shakahola sawa na eneo la Kwa Binzaro kupitia mafunzo ya dini potofu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

IEBC yasistiza usalama kwenye maandalizi ya uchaguzi mkuu

Published

on

By

Mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC, Erastus Ethekon, amesisitiza umuhimu wa usalama katika maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2027.

Akizungumza kwenye mkutano wa ushirikiano na vitengo vya usalama kutoka kaunti za Mombasa, Kwale na Kilifi, Ethekon alisema tume ya IEBC imeendelea kushirikiana kwa karibu na vitengo hivyo tangu mwaka 2013, kuhakikisha chaguzi zinakuwa za amani, haki na uwazi.

Hata hivyo Ethekon alikiri kuwepo kwa changamoto kama vile uhaba wa fedha, vitisho vipya vya kiusalama, ukiukaji wa haki za binadamu, pamoja na ghasia za kijinsia dhidi ya wanawake na wasichana wakati wa chaguzi.

Mwenyekiti huyo vile vile alisema usalama wa uchaguzi si wa siku ya kupiga kura pekee, bali ni mchakato unaopaswa kuzingatiwa kuanzia usajili wa wapiga kura hadi kutangazwa kwa matokeo.

Kwa upande wake, kamishna wa IEBC Anne Nderitu alisema tume ya IEBC imeweka mikakati kuhakikisha chaguzi ndogo zipatazo 24, zinafanyika kwa uwazi na kwa kuzingatia sheria.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike alimhukumu Lucky Munga na Hassan Daniel kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya Mahakama kubaini kwamba walihusika kwa kuwatendea unyama watoto wa umri wa miaka 13 na 15.

Safari Karisa Lewa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kumnajisi mtoto wake mwenyewe wa umri wa miaka 14 huku Eric Ruwa na Lucky Katana Kenga wakihukumiwa kifungo cha miaka 6 gerezani kwa kosa sawa na hilo.

Hata hivyo Mahakama hiyo ilimhukumu kifungo cha miaka 3 Kithi Kombe kutokana na kesi hiyo kwa mtoto wa miaka 15, japo baadaye Mahakama ikabaini kwamba mshukiwa sio baba halali wa mtoto aliyezaliwa baada ya Kithi kumnajisi mtoto huyo.

Akizungumza wakati wa vikao vya Mahakama baada ya kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisema Mahakama umezingatia ushahidi uliyotolewa Mahakamani huku akiwarai wananchi kujitenga na visawishi vibaya ili kuepuka mkono wa sheria.

Hakimu Wasike alihoji kwamba washtakiwa wa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama lakini kwa kuzingatia taratibu zote za Mahakama na sheria.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Trending