Sports
Viwanja Vya Kenya Kasarani, Nyayo Tayari Kwa Kipute Cha Chan
Mawaziri wawili waziri wa Michezo Salim Mvurya na waziri wa Usalama wa ndaani Kipchumba Murkomen wamethibitisha kwa pamoja viwanja vitakavyotumika kwa mtanange wa CHAN viko tayari.
Wakizungumza baada kuzuru uga wa Kasarani wawili hao wameweka wazi ubora wa viwanja hivyo viwili huku Mvurya akifichua kwamba kazi ya kuweka kanopi katika uga wa Nyayo kwa AFCON mwaka 2027 baada ya kukamilika kwa CHAN.
Kipute hicho kinangoa nanga mwezi ujao Agosti 2 ugani Benjamin Mkapa kabila ya fainali ugani Kasarani.