News

Duale, asitisha huduma za vituo vya afya 40 kwa udanganyifu wa SHA

Published

on

Waziri wa afya nchini Aden Duale amethibitisha kusitishwa kwa shughuli za vituo 40 vya afya ambavyo vilibainika kujihusisha na udanganyifu dhidi ya mamlaka ya bima ya afya ya SHA.

Akizungumza jijini Nairobi, Duale alisema usitishaji huo umeanza kutekelezwa mara moja na katika kipindi cha uchunguzi vituo hivyo havitapokea fedha zozote kutoka kwa SHA na vitawajibishwa kwa kurejesha fedha zilizopotea.

Vilevile, wizara hiyo iliwatambua wahudumu kadhaa wa afya ambao walihusika katika ufisadi na ubadhirifu wa raslimali za serikali wakiwemo madaktari 8 kutoka maeneo ya Bungoma, Nairobi na Kilifi.

Wizara ya afya haitaruhusu visa kama hivyo kuendelezwa kwenye vituo vya afya nchini na watakabiliwa kisheria’’ Alisema Duale
Duale pia alisema mikakti thabiti imewekwa kuhakikisha sekta ya afya nchini inaimarishwa vilivyo.

Taarifa ya Janet Mumbi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version