News
Viongozi wa upinzani waendelea kuisuta serikali
Viongozi wa upinzani wameikosoa serikali kwa kukosa kutekeleza ahadi walizotoa kwa wananchi hasa katika kufufua miradi ya kiuchumi nchini.
Wakiungumza katika kaunti ya Kakamega viongozi hao wakiongozwa na kinara wa Chama cha DCP Rigathi Gachagua waliomba wakaazi kushirikiana na kuiondoa serikali katika uchaguzi mkuu ujao.
Viongozi hao walimshtumu Rais William Ruto pamoja na kinara wa chama cha ODM Raila Odinga kwa kile walichosema ni kuwatelekeza wakaazi wa ukanda wa magharibi kila msimu wa baada ya uchaguzi mkuu.
“Nyinyi mnampatia kura anatoa fujo, anaitwa, anaingia kwa serikali anawaacha nyinyi kwa mataa, sasa mimi nimefukuza Ruto kule kwa mlima, nimefunga mlima kifunguo iko hapa kwa gari”,alisema Gachagua.
Kwa upande wake kinara wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka alieleza matumaini ya ushirikiano wao na Gachagua, akisema wanaamini wakipata uungwaji mkono wa wananchi wanambandua rais Ruto mamlakani.
Viongozi hao wanasema serikali imeshindwa kudhibiti taifa hasa kupunguza gharama ya maisha na kutimiza ahadi ya miradi ya maendeleo ya kufaidi mahasla.
“Sisi tumekosana na William Ruto kwa sababu ule mkataba ambao tuliandishana naye kama watui wa mkoa wa magharibi amekataa”,alisema Cleophas Malala.
Taarifa ya Joseph Jira.