News

Vijana eneo la Junju, Kilifi wavuna wasipopanda

Published

on

Maafisa wa Idara ya utawala wa mkoa katika wadi ya Junju kaunti ya Kilifi imeonya wakaazi wa kijiji cha Mwembetsungu dhidi ya kuendekeza visa vya wizi.

Hii ni baada ya mwanamke mmoja kunusurika kifo mikononi mwa wakaazi waliokuwa na gadhabu baada ya kumfumania akiiba mahindi kwenye shamba moja kijijini humo.

Mzee wa Mtaa kwenye kijiji hicho Elijah Mbigo alisema visa vya wizi wa mahindi kijijini humo vimekithiri mno msimu huu, huku akitaja kufikia sasa zaidi ya mashamba matano yamevamiwa na mahindi kuibiwa.

Akiongea na coco fm, Mbigo aliweka wazi kwamba tayari mikakati ya kukabiliana na wizi huo imewekwa huku akiwataka wakaazi wa kijiji hicho kushirikiana ili kuhakikisha wanaotekeleza wizi huo wanapatikana na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

“Onyo ninatoa kila siku lakini bado halijazingati kwa sababu vijana hapa niwavivu hawataki vibarua, hata wakiitwa kazi mahali hawaendi, sasa hiyo inafanya mtaa umeharibika kwa sababu ya uvivu wa vijana”, alisema Mbigo.

Kauli yake iliungwa mkono na mzee wa nyumba kumi kwenye kijiji hicho Benson Mganga ambaye alisisitiza haja ya ushirikiano miongoni mwa wakaazi huku akitaka sheria kali kuchukuliwa endapo wanaotekeleza wizi huo watapatikana.

Taarifa ya Mwanahabari wetu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version