Connect with us

News

Vijana eneo la Junju, Kilifi wavuna wasipopanda

Published

on

Maafisa wa Idara ya utawala wa mkoa katika wadi ya Junju kaunti ya Kilifi imeonya wakaazi wa kijiji cha Mwembetsungu dhidi ya kuendekeza visa vya wizi.

Hii ni baada ya mwanamke mmoja kunusurika kifo mikononi mwa wakaazi waliokuwa na gadhabu baada ya kumfumania akiiba mahindi kwenye shamba moja kijijini humo.

Mzee wa Mtaa kwenye kijiji hicho Elijah Mbigo alisema visa vya wizi wa mahindi kijijini humo vimekithiri mno msimu huu, huku akitaja kufikia sasa zaidi ya mashamba matano yamevamiwa na mahindi kuibiwa.

Akiongea na coco fm, Mbigo aliweka wazi kwamba tayari mikakati ya kukabiliana na wizi huo imewekwa huku akiwataka wakaazi wa kijiji hicho kushirikiana ili kuhakikisha wanaotekeleza wizi huo wanapatikana na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

“Onyo ninatoa kila siku lakini bado halijazingati kwa sababu vijana hapa niwavivu hawataki vibarua, hata wakiitwa kazi mahali hawaendi, sasa hiyo inafanya mtaa umeharibika kwa sababu ya uvivu wa vijana”, alisema Mbigo.

Kauli yake iliungwa mkono na mzee wa nyumba kumi kwenye kijiji hicho Benson Mganga ambaye alisisitiza haja ya ushirikiano miongoni mwa wakaazi huku akitaka sheria kali kuchukuliwa endapo wanaotekeleza wizi huo watapatikana.

Taarifa ya Mwanahabari wetu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mabadiliko ya tabianchi yatajwa kuchangia mapato duni ya samaki, Lamu

Published

on

By

Wadau katika sekta ya mazingira kaunti ya Lamu wanasema mabadiliko ya hali ya anga yanayoshuhudiwa sawa na ujenzi wa bandari ya Lamu kumechangia mapato ya samaki kupungua katika bahari hindi.

Mahmoud Yusuf ambaye ni mwanazingira alisema zana za kizamani wanazotumia wavuvi kuvua samaki pia zinachangia mapato duni ya samaki.

Yusuf alisema tangu ujenzi huo wa bandari uanze, maji ya bahari chini yamekuwa na matope kutokana na kuchimbwa na kufukuliwa kwa bahari, hali iliyochangia samaki kutorokea bahari kuu.

Mwanamazingira huyo aliitaka serikali kuwapa wavuvi vifaa vya kisasa vya uvuvi sawa na meli za uvuvi zitakazowawezesha kufika maji makuu, baada ya bandari ya ndani kuharibika.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Gachagua atangaza azma ya kuwania urais 2027

Published

on

By

Kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua ametangaza nia ya kuwania wadhfa wa urais mwaka 2027 akilenga kumg’oa rais William Ruto mamlakani.

Gachagua amekuwa akifanya ziara katika eneo la mlima kenya pamoja na viongozi wa chama chake akitumia mikutano ya barabarani kutangaza azma yake ya kuwania urais.

Kulingana na Gachagua serikali ya sasa inatumia mikutano ya ikulu kuendeleza vitendo vya ufisadi, na ameahidi kuwa akichaguliwa atakomesha matumizi mabaya ya fedha za umma.

Katika ziara hiyo viongozi wa chama chake walieza kuwa Gachagua ndiye mgombea anayefaa kupeperusha bendera ya upinzani, wakidai eneo la mlima kenya limejiondoa katika uungwaji mkono wa serikali ya sasa.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

Trending