Sports
Timu Za Kenya Mpira Wa Hoki Zajianda Mechi Za Bara Afrika
Timu za Kenya upande wa akina dada na wanaume mpira wa Hoki zimezidi kujitia makali ugani City Park Nairobi tayari kwa mashindano ya Kombe la Bara Afrika mjini Ismaella Misri Oktoba 11-18.
Vikosi vyote vimakua na zaidi ya mazoezi ya mara tatu kwa siku wakilenga kuandikisha matokeo ya kuridhisha katika makala ya mwaka huu.
Kulingana na kocha wa Akina dada Meshack Senge wanajinoa zaidi ili kuboresha matokeo walioandikisha mwaka 2022 mjini Accra Ghana.
Katika makala ya mwaka 2022 katika Taifa la Ghana Kenya ilijinyakulia taji la Shaba kwa akina dada huku wenyeji Ghana wakimaliza nafasi ya Tatu nayo Misri nafasi ya kwanza na kushinda Dhahabu.