Sports
Timu Za Kenya Mpira Wa Hoki Zajianda Mechi Za Bara Afrika

Timu za Kenya upande wa akina dada na wanaume mpira wa Hoki zimezidi kujitia makali ugani City Park Nairobi tayari kwa mashindano ya Kombe la Bara Afrika mjini Ismaella Misri Oktoba 11-18.
Vikosi vyote vimakua na zaidi ya mazoezi ya mara tatu kwa siku wakilenga kuandikisha matokeo ya kuridhisha katika makala ya mwaka huu.
Kulingana na kocha wa Akina dada Meshack Senge wanajinoa zaidi ili kuboresha matokeo walioandikisha mwaka 2022 mjini Accra Ghana.
Katika makala ya mwaka 2022 katika Taifa la Ghana Kenya ilijinyakulia taji la Shaba kwa akina dada huku wenyeji Ghana wakimaliza nafasi ya Tatu nayo Misri nafasi ya kwanza na kushinda Dhahabu.
Sports
Harambee Stars Kundi La Kifo Kundi B.

Sports
Kiungo Wa Brenford Bryan Mbeumo Sasa Ni Mali Ya United

Baada ya vute ni kuvute ambayo imedumu kwa kipindi cha mwezi mmoja ni rasmi kwamba kilabu ya manchester United na Brenford wameafikia makubaliano ya pauni milioni 70 ya kiungo mshambulizi Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.
Haya yanajiri baada ya ofa mara mbili ya united kukataliwa na kilabu hio kabila ya kutuma ofa ya mwisho ya pauni milioni 65 na nyongesa ya pauni milioni 5.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano baada kukubali matakwa yake binafsi.
Mbeumo anakua sajili wa pili kwa kocha mkuu Ruben Amorim baada ya ujio wa mshmabulizi Matheus Cunha.