News

Rais Ruto aahidi kusaidia sekta ya Boda Boda

Published

on

Rais William Ruto amesema atawasilisha bungeni pendekezo la kupunguzwa kwa ushuru wa pikipiki ili kuwawezesha vijana kote nchini kuwa na uwezo wa kumiliki pikipiki na kujiimarisha kiuchumi.

Rais Ruto alisema japo kwa sasa bei ya pikipiki hizo imeshuka, jukumu la serikali ni kuhakikisha vijana wanakuwa na uwezo wa kujiimarisha kiuchumi na hatua hiyo itaafikiwa kwa kupunguzwa kwa ushuru wa pikipiki.

Akizungumza katika Ikulu ya Nairobi baada ya kukutana na viongozi wa wahudumu wa bodaboda kote nchini, rais Ruto alisema mpango huo utahakikisha mwananchi wa kawaida anamiliki pikipiki kwa kulipia kiwango cha chini zaidi cha shilingi 9,500.

Kiongozi wa nchi, aliwarai vijana kukumbatia mpango huo kwani nia yake ni kuwawezesha vijana kuzikabili changamoto mbalimbali za kimaisha sawa na kudhibiti uchumi wa taifa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version