News

Mwambire: Mahakama za Ardhi Zinafaa Kuzuru Mashinani

Published

on

Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi Teddy Mwambire amezitaka Mahakama zinazoshuhulikia mizozo ya Ardhi na Mazingira nchini kufanya uchunguzi wa kina wa kesi za mizozo ya ardhi katika kaunti za Pwani kabla ya kutoa uamuzi.

Mwambire amependekeza Mahakama hizo kuzuru nyanjani kwenye ardhi zilizo na migogoro ili kubaini changamoto zinazochangia mizozo hiyo, akisema baadhi ya wanunuzi wa ardhi hufanya ununuzi wakiwa mbali bila ya kutathimini ardhi wanazouziwa.

Akizungumza na Mwambire ameitaja hatua hiyo kama itakayowezesha Mahakama kutoa uamuzi bila ya kuegemea upande wowote.

Kulingana na Spika Mwambire, baadhi ya uamuzi ambao umekuwa ukitolewa na Mahakama kuhusu kesi za mizozo ya ardhi mara nyingi umekuwa ukichangia mgawanyiko na mizozano migogoro mwa jamii.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version