News

Muturi Apokonywa Walinzi wake

Published

on

Aliyekuwa Waziri wa utumishi wa umma nchini Justin Muturi amesema maisha yake yamo hatarini baada ya kupokonywa walinzi wake ambao aliyokuwa nao tangu akiwa Spika wa bunge la kitaifa.

Katika kikao na Wanahabari, Muturi amesema walinzi wake wawili waliagizwa kuondoka katika makaazi yake mwendo wa saa moja na nusu usiku, siku ya Jumatatu.

Muturi amesema walinzi hao walimwambia kwamba waliagizwa kutoendeleza majukumu yao ya ulinzi kutokana na mvutano kati yake na serikali, akisema hatua hiyo inalenga kumkandamiza kisiasa.

Muturi amehoji kwamba japo hana wasiwasi wote kuhusu swala hilo lakini usalama wake ni muhimu huku akisema serikali imegonga sipo kwani atahakikisha anawaeleza wakenya ukweli kuhusu madhila ya serikali.

Itakumbukwa kwamba Muturi alitimuliwa kazini na Rais William Ruto kutokana na msimamo wake wa kuikosoa serikali kufuatia visa vya utekaji nyara na mauaji ya kiholela, ufisadi ndani ya serikali pamoja na kudhalilishwa kwa mawaziri nchini.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version