News

Mahakama ya Mombasa Kusikiliza Kesi ya Mauaji ya Afisa wa IEBC

Published

on

Mahakama kuu ya Mombasa imeanza kuskiliza kesi ya mauaji ya aliyekuwa Kaimu Meneja wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC katika kaunti ya Kilifi Aisha Akinyi Abubakar.

Washtakiwa katika kesi hiyo, Joseph Sunday Otieno maarufu Brian Shikuku na Brian Templer Oyare wanakabiliwa na tuhuma za mauaji ya afisa huyo nyumbani kwake katika mtaa wa Utange eneo bunge la Kisauni katika kaunti ya Mombasa mnamo mwezi Januari tarehe 5 mwaka huu.

Wawili hao pia walishtakiwa kwa kosa la kumpiga na kumjeruhi Mwanawe Marehemu na kutoweka na vifaa vya kieletroniki ikiwemo simu na vifaa vya IEBC, nyumbani kwao wakati wa tukio hilo.

Jaji Wendy Micheni ameanza kusikiliza kesi hiyo baada ya vipimo vya kiafya kutoka kwa madaktari kubaini kwamba washukiwa hao wawili wana akili timamu, hii ni baada ya Mahakama hapo awali kuagiza washukiwa hao wafanyiwe vipimo vya afya akili.

Oyare na Otieno wataendelea kufuatilia vikao vya kesi hiyo wakiwa rumande baada ya Mahakama kuwanyima dhamana kutokana na mashtaka yanayowakabili.

Kesi hiyo itaendelea kesho katika Mahakama hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version