News

Mahakama ya Kisutu nchini Tanzania imeahirisha kesi Lissu

Published

on

Mahakama ya Kisutu nchini Tanzania imeahirisha kesi ya jinai inayomkabili Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu hadi Juni 16, 2025.

Mahakama imeagiza Lissu kuendelea kuzuiliwa rumande.

Uamuzi huo umetolewa baada ya kesi yake kutajwa Mahakamani ambapo upande wa serikali imeomba Mahakama kuupa muda zaidi ili kukamilisha uchunguzi dhidi ya mashtaka yanayomkabili Lissu.

Lissu anakabiliwa na mashtaka mbalimbali ikiwemo kosa la uhaini huku kesi hiyo ikifuatiliwa kwa karibu na umma kupitia matangazo ya moja kwa moja. 

Mwenyekiti wa chama cha CHADEMA Tundu Lissu

Lissu ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama cha upinzani nchini Tanzania CHADEMA alikamatwa mwezi Aprili mwaka huu mkoani Ruvuma na kushtakiwa kwa tuhuma za uhaini na kuchapisha taarifa za uongo.

Mawakili wa Lissu wamewasilisha malalamiko kwa Umoja wa Mataifa wakitaka kutangazwa kwa kukamatwa na kuzuiliwa kwa Lissu kuwa kinyume cha sheria, wakisema mashtaka hayo yamechochewa kisiasa na yanalenga kumzuia Lissu kushiriki uchaguzi mkuu ujao utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka 2025.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version