News
Kina mama wajawazito na waliojifungua kwenye hospitali ya rufaa mjini Kilifi, wapokea zawadi kutoka Coco Fm
Uhaba wa wauguzi ni miongoni mwa changamoto ambazo zinatatiza shughuli za utoaji wa huduma za matibabu katika hospitali ya rufaa mjini Kilifi kaunti ya Kilifi.
Wakizungumza na Coco Fm, baadhi ya wauguzi wa hospitali ya rufaa Mjini Kilifi wakiongozwa na Nyadzua Pandau wamesema hali hiyo inawafanya kulazimika kufanya kazi kupita muda unaohitajika kwani idadi ya wagonjwa wanaohitaji matibabu ni kubwa kuliko ile ya wauguzi waliopo kwenye hospitali hiyo.
Vilevile, wametaja ukosefu wa dawa kwenye hospitali hiyo na kutoa wito kwa serikali ya Kaunti ya Kilifi kuhakikisha zinapatikana ili wagonjwa watibiwe bila changamoto zozote.
Aidha, wauguzi hao wameitaka serikali ya kitaifa pamoja na ya kaunti ya Kilifi kuwekeza zaidi katika kuimarisha huduma za matibabu na kukishukuru kituo cha COCO FM kwa kutoa zawadi kwa kina mama hospitalini humo jana wakati wa siku ya Kina duniani.
Thomaskombe
May 13, 2025 at 1:28 pm
Coco fm radio ina matangazo bora
Twaomba itufikie huku mitaani kweku
Magarini naviungani maana tuna hitaji matangazo na burudani
Na vipindi vya salamu