News

Kina mama wajawazito na waliojifungua kwenye hospitali ya rufaa mjini Kilifi, wapokea zawadi kutoka Coco Fm

Published

on

Uhaba wa wauguzi ni miongoni mwa changamoto ambazo zinatatiza shughuli za utoaji wa huduma za matibabu katika hospitali ya rufaa mjini Kilifi kaunti ya Kilifi.

Wakizungumza na Coco Fm, baadhi ya wauguzi wa hospitali ya rufaa Mjini Kilifi wakiongozwa na Nyadzua Pandau wamesema hali hiyo inawafanya kulazimika kufanya kazi  kupita muda unaohitajika kwani idadi ya wagonjwa wanaohitaji matibabu ni kubwa kuliko ile ya wauguzi waliopo kwenye hospitali hiyo.

Vilevile, wametaja ukosefu wa dawa kwenye hospitali hiyo na kutoa wito kwa serikali ya Kaunti ya Kilifi kuhakikisha zinapatikana ili wagonjwa watibiwe bila changamoto zozote.

Aidha, wauguzi hao wameitaka serikali ya kitaifa pamoja na ya kaunti ya Kilifi kuwekeza zaidi katika kuimarisha huduma za matibabu na kukishukuru kituo cha COCO FM kwa kutoa zawadi kwa kina mama hospitalini humo jana wakati wa siku ya Kina duniani.

 

0 Comments

  1. Thomaskombe

    May 13, 2025 at 1:28 pm

    Coco fm radio ina matangazo bora
    Twaomba itufikie huku mitaani kweku
    Magarini naviungani maana tuna hitaji matangazo na burudani
    Na vipindi vya salamu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version