News

KMPDU yaonya madaktari wazembe pwani

Published

on

Muungano wa madaktari nchini KMPDU tawi la pwani umeonya madaktari wazembe ukisema hautamtetea daktari yeyote atakayepatikana anakwepa majukumu yake.

Hii ni baada ya taarifa ya kamati ya afya ya bunge la seneti katika ziara yao kwenye hospitali ya rufaa ya Kilifi, kudai walikosa kuwaona baadhi ya madaktari waliopaswa kuwa kazini wakati huo.

Mwenyekiti wa KMPDU eneo la Pwani Daktari Niko Gichana alisema usimamizi wa kaunti unafaa kueleza chanzo cha madaktari hao kutokuwa kazini.

Gichana aliongeza kuwa hospitali za umma zinakumbwa na uhaba mkubwa wa madaktari na kusababisha waliopo kufanya kazi kwa mda mrefu bila mapumziko.

Afisa huyo alishauri usimamizi wa kaunti ya Kilifi kushughulikia suala la uajiri wa madaktari zaidi.

Kamati hiyo ikiongozwa na seneta David Wakoli Wafula ilibaini kuwepo dawa za matibabu zilizopitwa na wakati, baadhi ya madaktari kutofika kazini pamoja na hali duni ya usafi hospitalini wakati ilipozuru taasisi hiyo ya afya.

Ilimtaka gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro kuwachukulia hatua za kinidhamu wahudumu wa afya waliokwepwa majukumu.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version