News

Kikao cha umma chazua mvutano Msambweni

Published

on

Mkutano wa ukusanyaji maoni ya umma kaunti ya Kwale kuhusiana na pendekezo la kuongezwa kwa ada za kuingia katika mbuga za wanyamapori nchini uliibua hisia mseto miongoni mwa wenyeji wa kaunti ya Kwale.

Mkutano huo ulioandaliwa na Shirika la huduma kwa wanyamapori nchini KWS eneo la Bongwe ulitibuka baada ya viongozi wa kisiasa na wakaazi wanaoendeleza shughuli zao katika fuo za bahari kudai kuwa serikali ina njama ya kunyakuwa eneo la Diani Chale Marine Reserve.

Wakiongozwa na mbunge wa Msambweni kaunti ya Kwale Feisal Bader, Madai ya wakaazi hao yalijiri kufuatia tangazo la hapo awali lililochapishwa kwenye gazeti rasmi la serikali kuwa eneo hilo linafaa kuwa katika himaya ya KWS.

“Sisi kama Wananchi wa Msambweni tunasema maoni yetu tunayatoa kuwa tunaanza rasmi mchakato kuhusu eneo la Diani Marine reserve’’, alisema Bader.

Mbunge wa Msamweni Feisal Bader akihutubia wakaazi wa Msambweni

Hata hivyo naibu Mkurugenzi wa uhifadhi eneo la Pwani Elema Hapisha alisema shughuli hiyo inayoendelea katika maeneo tofauti nchini haihusiani kivyovyote na utata unaojiri kuhusu usimamizi wa eneo la Diani Chale Marine Reserve.

Taarifa ya Janet Mumbi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version