News
Gavana Mung’aro aapa kukabiliana na matabibu wazembe
Gavana wa kaunti ya Kilifi Gideon Maitha Mung’aro amesema muungano wa madaktari nchini KMPDU umekua kikwazo kikubwa katika kulainisha utendakazi wa madaktari.
Gavana Mung’aro alisema muungano huo wa kutetea maslahi ya madaktari nchini umelemaza huduma za matibabu hasa katika hospitali za umma.
Akizungumza na wanahabari katika makaazi yake, gavana Mung’aro alitishia kuwachukulia hatua kali madaktari wazembe na wale wanaosusia kazi mara kwa mara huku wakihudumu katika hospitali za kibinafsi.
Vile vile gavana huyo aliokeza kuwa wizara ya afya inalenga kuajiri madakrati wa kliniki wapya ili kukabiliana na changamoto hiyo.
Haya yanajiri baada ya kamati ya afya ya bunge la seneti kuzuru hospitali ya rufaa ya Kilifi mjini Kilifi na kuwakosa baadhi ya madaktari waliopaswa kuwa kazini.
“Mimi mwenyewe sikwenda pamoja na nyinyi wakati mlikua mnatembelea hospitali hizo lakini nafurahi kwa sababu mmejionea wenyewe kwamba matabibu wengi wanafanya kazi katika hospitali za kibinafsi wanakuja kazini pindi tu wanapopigiwa simu kwamba kuna mgonjwa, na nitahakikisha imekomesha hii tabia”, alionya gavana Mung’aro.
Taarifa ya Elizabeth Mwende