Sports

Finali Ya Euro Ya Akina Dada Ni Kati Ya Uhispania Na Uingereza Jumapili

Published

on

Timu ya Taifa ya Wanawake ya Uhispania imetinga fainali ya kombe la Mataifa ya Ulaya kwa Wanawake mwaka 2025, WEURO 2025 kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Ujerumani katika dimba la Letzigrund mjini, Zürich kwenye nusu fainali.

Timu zote mbili zilikosa nafasi kochokocho za kufunga katika mchezo huo huku Uhispania wakilenga zaidi ya mashuti 10 langoni ila haikuzaa matunda katika dakika 90 za mchezo.

Mchezo huo ulilazimika kuamuliwa kwenye muda wa ziada ambapo mshambulizi wa Barcelona Aitana Bonmati alifunga goli la kipekee dakika ya 113 baada ya dakika 90 kumalizika bila bao.
Uhispania itachuana na Mabingwa watetezi, England kwenye fainali siku ya Jumapili.
England waliwabandua Italia magoli 2-1 katika nusu fainali ya kwanza siku ya Jumanne.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version