News

Fikirini Jacobs: Serikali kuimarisha vijana kibiashara

Published

on

Katibu katika idara ya vijana na uchumi bunifu nchini Fikirini Jacobs amesema serikali imeweka mikakati kabambe ya kubuni ajira kwa vijana kupitia miradi ya kibiashara.

Akizungumza na Coco Fm, Jacobs alisema vijana ambao hawakamilisha elimu ya sekondari, wameangaziwa katika mradi wa kibiashara uitwao Nyota ambao serikali imeekeza pesa za kutosha.

Jacobs amedokeza kuwa mpango huo unaolenga vijana 100,000 utazinduliwa hivi karibuni nchini na vijana 70 katika kila wadi nchini watafaidi.

Alidokeza kuwa tayari idadi kubwa ya vijana wametuma maombi ya kusajiliwa katika mpango huo.

“Sehemu ya kwanza kutegemea na vile ambavyo zilitangazwa inaitwa Business Support, ni sehemu ambayo mhesimiwa rais alitangaza hata akiwa siku ya madaraka kule Homabay kwamba kumewekwa shilingi bilioni tano kati ya hizi bilioni zote ambazo lengo lake ni kuenda kusaidia vijana laki moja ambao ni vijana 70 kwa kila wadi ya Kenya”, alisema Fikirini

Pia alisema kuwa vijana wanaoishi na ulemavu nchini wamezingatiwa katika mpango huo katika juhudi za kuafikia usawa.

Vile vile alisema serikali imejenga vituo 155 vya kuwezesha kiujuzi vijana katika maeneo bunge yote nchini akidokeza kuwa kaunti ya Kilifi kuna vituo viwili zaidi ambavyo vitajengwa.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version