Sports
Kocha Wa Ureno Jose Mourinho Apigwa Kalamu na Fernabache Ya Uturuki
Mkufunzi wa Ureno Jose Mourinho ametimuliwa na klabu ya Fenerbahce ya Ligi Kuu ya Uturuki baada ya michezo sita pekee tangu kuanza kwa msimu mpya.
Sababu kuu ya hatua hiyo ilikuwa ni kichapo dhidi ya Benfica Jumatano usiku, kilichosababisha Fenerbahce kukosa kufuzu kwa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa.
Taarifa kwenye akaunti rasmi ya Fenerbahce katika X ilisomeka: “Timu yetu ya Soka ya Kitaaluma imeachana na Jose Mourinho, ambaye amekuwa kocha mkuu tangu msimu wa 2024-2025. Tunamshukuru kwa juhudi zake kwa timu yetu hadi sasa na tunamtakia mafanikio katika taaluma yake ya baadaye.”
Mourinho, mwenye umri wa miaka 62, aliteuliwa kuwa meneja wa Fenerbahce mwezi Mei 2024, akitia saini mkataba wa miaka miwili. Hata hivyo, kipigo cha 1-0 katika uwanja wa Estadio da Luz kimefupisha muda wake nchini Uturuki.
Kwa mujibu wa jarida la michezo la Uturuki, Spor Arena, uhusiano wa Mourinho na bodi ya Fenerbahce ulikuwa na misukosuko wakati wa dirisha la usajili la kiangazi, huku kocha huyo wa zamani wa Manchester United akikosoa mkakati wa klabu hiyo.
Kocha huyo amewahi kuvinoa pia vilabu vya Chelsea,Manchester United,Spurs,Real na As Roma.