Sports

Kocha Wa Gor Zico Ataka Mashemeji Derby zichezwa Nje ya Nairobi

Published

on

Mkufunzi mshikilizi wa kilabu ya Gor Mahia Zedekiah Zico Otieno amesema kwamba ni wakati mwafaka kwa mechi nyingi za debi la Mashemeji kati mahasimu wa tangu jadi Gor na Afc Leopards zichezwe nje ya mji wa Nairobi.

Mwalimu huyo aliysema hayo kwenye kikao na wanahabari ambapo amesema kwamba itakua ni raha kuona mechi hiyo ikichezwa Kakamega,Mumias au hata Busia miaka zijazo.

Hayo yanajiri huku Zico akiweka wazi wanakwenda uwanjani Raila Odinga katika kaunti ya Homabay kusaka alama tatu muhimu siku ya jumatano dhidi ya Afc Leopards.

“Nadhani itakua ni mechi mgumu kwani debi haijakua rahisi ila tunakwenda kusaka alama tatu muhimu na kupunguza mwanya kati yetu na wapinzani wetu,ndaani ya Kogalo tunajua ushindi tu na najua mashabiki wanataka hilo,lengo letu ni ushindi tu siku ya Jumatatu.”

Tiketi za mchuano huo zinauzwa kwa shilingi 300 mshabiki wa kawaida huku mashabiki mashuhuri wakilipia shilingi 3000.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version