News
Wachezaji 3 Kumkaba Yamal Leo Kilabu Bingwa
Mkufunzi wa kilabu ya Inter Milan ya Italia Simeone Inzaghi amesema kwamba mechi ya leo kati yao na Fc Barcelona ni kufa kupona wakilenga tiketi ya kufuzu fainali ya kilabu bingwa ulaya mei 31 uwanjani Allianz Arena.
Akizungumza saa chache kabla ya mtanange huyo mwalimu huyo aidha amekiri ili kushinda mechi hiyo ni lazima wapate mbinu ya kuwazuia vizuri wapinzani wao kwa ustadi mkubwa la si hivyo watawadhuduru.
Miongoni mwa mikakati ambayo ameweka kocha huyo ni wachezaji watatu kumdhibiti winga matata na tineja Lamine Yamal mwenye umri wa miaka 17.
Kwa mujibu wa kocha huyo kama kuna mchezaji atasaidia Barcelona kuingia fainali basi ni makali ya mhispanyola Yamal,mchezaji huyo fundi alifunga goli kabla ya kuchangia lingine timu hizo ziktoka sare ya magoli 3-3 ugani stade olympique st.luis catalunya.
Na Simeone amesisitiza ni lazima wasimpe nafasi tineja huyo akitaka wachezaji watatu wawe naye anashika mpira.
Mechi hiyo inapigwa majira saa nne usiku Jumanne hii Ugani Sansiro Italia.