News
Manchester United Guu Moja Fainali Europa
Miamba wa Uingereza kilabu ya manchester united imeweka guu moja fainali ya UEFA Europa Ligi baada ya ushindi wao mnono wa magoli 3-0 dhidi ya Athletic Bilbao ugani san mames uhispania.
Kiungo wa taifa la Brazil Casemiro aliwaweka uongozi Mashetani wekundu kunako dakika 30 kipindi cha kwanza kabla ya nahodha Bruno Fernandes kuongeza goli la pili dakika ya 37 huku akifunga lingine na lake la pili dakika ya 45 kupitia tuta au penalty.
Kilabu ya Bilbao walimaliza wachezaji 10 baada ya kadi nyekundu kwa beki wake Dani vivian dakika ya 35. kwenye mechi nyingine Tottenham Hotspurs walicharaza Bodo/Glimt ya Norway magoli 3-1.
Kwenye taji la Uefa Conference ligi kilabu ya Chelsea ilichapa Djugarden ya uswedi magoli 4-1 nayo Real Betis ya Uhispania ikichakaza Fiorentina ya Italia magoli 2-1 .
Mechi za mkondo wa pili utapigwa Alhamisi ijayo ugani Old Trafford ambapo Bilbao itahitaji kuwafunga United magoli 4-0 ili kufuzu kwenye fainali Mei 21.