News

Tuko Tayari Kufuzu Kombe La Dunia

Published

on

Nahodha wa Kikosi cha Soka vijana chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20 Rising Stars Amos Wanjala amesema kwamba lengo lao kuu ni kufuzu kombe la dunia kwenye fainali ya mashindano ya Afcon kwa chipukizi iliofungua milango yake weikndi hii mjini Cairo Misri.

Akizungumza akiwa kambini mjini Cairo Wanjala anamini kwamba wana kikosi bora cha kuandikisha matokeo chanya kwenye kombe hilo licha ya kuwa ni mara yao ya kwanza kushiriki katika kipute hicho.

“Tuko tayari kufuzu World cup maana tumekua tukijiandaa vyema kwa mashindano haya,nataka niwatoe hofu wakenya kwamba kundi letu ni la kifo kwani wawe tayari kupata burudani kutoka kwetu.”

kwa Mujibu wa tineja huyo wa academia ya Nasty Sports ya Uhispania ni kwamba licha mabadiliko ya hali ya anga akilinganisha na Kenya kila mmoja yuko tayari kuonyesha uwezo wake katika jukwaa hili.

“Tuko syched up kucheza na mpinzani yeyote,kila mmoja amejiandaa vizuri kutendea haki na kupeperusha bendera ya taifa letu. Nikitaka kushukuru wizara ya michezo pamoja na shirikisho kwa kutuunga mkono kuanzia mwanzo wa mazoezi yetu mpaka mandhari ambayo tumepata hapa.”

Vijana wa nyumbani wanafungua kampeni dhidi ya Morocco May 1 wakiwa kundi B pamoja na Tunisia na vilevile Nigeria

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version