Connect with us

News

Tuko Tayari Kufuzu Kombe La Dunia

Published

on

Nahodha wa Kikosi cha Soka vijana chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20 Rising Stars Amos Wanjala amesema kwamba lengo lao kuu ni kufuzu kombe la dunia kwenye fainali ya mashindano ya Afcon kwa chipukizi iliofungua milango yake weikndi hii mjini Cairo Misri.

Akizungumza akiwa kambini mjini Cairo Wanjala anamini kwamba wana kikosi bora cha kuandikisha matokeo chanya kwenye kombe hilo licha ya kuwa ni mara yao ya kwanza kushiriki katika kipute hicho.

“Tuko tayari kufuzu World cup maana tumekua tukijiandaa vyema kwa mashindano haya,nataka niwatoe hofu wakenya kwamba kundi letu ni la kifo kwani wawe tayari kupata burudani kutoka kwetu.”

kwa Mujibu wa tineja huyo wa academia ya Nasty Sports ya Uhispania ni kwamba licha mabadiliko ya hali ya anga akilinganisha na Kenya kila mmoja yuko tayari kuonyesha uwezo wake katika jukwaa hili.

“Tuko syched up kucheza na mpinzani yeyote,kila mmoja amejiandaa vizuri kutendea haki na kupeperusha bendera ya taifa letu. Nikitaka kushukuru wizara ya michezo pamoja na shirikisho kwa kutuunga mkono kuanzia mwanzo wa mazoezi yetu mpaka mandhari ambayo tumepata hapa.”

Vijana wa nyumbani wanafungua kampeni dhidi ya Morocco May 1 wakiwa kundi B pamoja na Tunisia na vilevile Nigeria

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Askofu Anyolo: Kadinali Njue Hatahudhuria Conclave

Published

on

By

Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Nairobi limetangaza kwamba John Kadinali Njue, hatashiriki Kongamano la kumchagua Papa mpya wa Kanisa Katoliki duniani.

Katika taarifa rasmi iliyotolewa na Kanisa hilo siku ya Jumanne, Kadinali Njue ambaye anastahili kupiga kura katika Kongamano hilo maarufu Conclave alikuwa amepokea mwaliko rasmi kutoka Shirika la kitume ili kuhudhuria Kongamano hilo ambalo linafaa kuanza rasmi tarehe 7 mwezi Mei mwaka huu lakini hataweza kusafiri.

Kanisa hilo limesema Mwakilishi wa Papa nchini Kenya Askofu Hubertus Marie Van Megen baada ya kushauriana na ofisi ya Askofu mkuu wa Nairobi Phillip Anyolo, alitoa taarifa kwamba Kadinali Njue mwenye umri wa miaka 80 hataweza kusafiri hadi Vatican- Roma kwa Kongamano hilo.

Picha kwa hisani

Askofu Anyolo amewataka waumini wa Kanisa Katoliki kuombea makadinali wanaochukua jukumu zito la kumchagua Papa mpya huku akihimiza maombi zaidi kwa ajali ya Afya na ustawi wa Kadinali Njue.

Continue Reading

News

Wachezaji 3 Kumkaba Yamal Leo Kilabu Bingwa

Published

on

By

Mkufunzi wa kilabu ya Inter Milan ya Italia Simeone Inzaghi amesema kwamba mechi ya leo kati yao na Fc Barcelona ni kufa kupona wakilenga tiketi ya kufuzu fainali ya kilabu bingwa ulaya mei 31 uwanjani Allianz Arena.

Akizungumza saa chache kabla ya mtanange huyo mwalimu huyo aidha amekiri ili kushinda mechi hiyo ni lazima wapate mbinu ya kuwazuia vizuri wapinzani wao kwa ustadi mkubwa la si hivyo watawadhuduru.

Miongoni mwa mikakati ambayo ameweka kocha huyo ni wachezaji watatu kumdhibiti winga matata na tineja Lamine Yamal mwenye umri wa miaka 17.

Kwa mujibu wa kocha huyo kama kuna mchezaji atasaidia Barcelona kuingia fainali basi ni makali ya mhispanyola Yamal,mchezaji huyo fundi alifunga goli kabla ya kuchangia lingine timu hizo ziktoka sare ya magoli 3-3 ugani stade olympique st.luis catalunya.

Na Simeone amesisitiza ni lazima wasimpe nafasi tineja huyo akitaka wachezaji watatu wawe naye anashika mpira.

Mechi hiyo inapigwa majira saa nne usiku Jumanne hii Ugani Sansiro Italia.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.