News

Mambo Atakia Kheri Rising Stars Misri Afcon u20

Published

on

Kiungo wa zamani timu ya taifa ya soka Harambee Stars Robert Mambo ametakia vijana wa timu chipukizi Rising Stars kila la kheri katika mashindano ya Afcon kwa chipukizi wakianza kampeini dhidi ya Morocco Mei 1.

Akizungumza kutoka Sweeden kupitia kanda ya video Mambo ameshukuru Rising Stars kupata nafasi hiyo ya kuakilisha taifa mjini Cairo akitaka wawe na ujasiri wasiogope timu yoyote.

“Kwanza Nishukuru Vijana wa Rising Stars pamoja na kocha Salim Babu,Hii ni fursa ya stars kuonyesha makali yao kwani mechi hizi ni kama mechi zingine,msiogope yeyote kwani tuna uwezo wa kushinda mtu yeyote kombe hili.”

Kulingana na Mambo ambaye kwa sasa amechukua mafunzo ya ukufunzi nchini Sweeden ni kwamba licha ya kundi hilo kuwa ngumu Rising stars hawafai kuonekana mnyonge hata kidogo kwa sababu wako kumi 11 uwnajani kama wenzao

“Msiogope yeyote kwani mmejitayarisha vya kutosha na ni muda wa kuenjoy na kushowcase vipaji vyenu kwa dunia. ” -Mambo.

Rising Stars wako kundi B pamoja na Morocco,Tunisia na Nigeria.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version