News

Kilabu Ya Barcelona Yakabwa Koo UEFA

Published

on

Miamba wa Uhispania kilabu ya Barcelona kina kibarua kigumu mechi ya mkondo wa pili nchini Italia baada ya kutoka sare ya magoli 3-3 dhidi ya Intermilan mechi ya mkondo wa kwanza ugani Estadio Olympic St.luis Companys siku ya jumatano.

Mshambulizi wa Ufaransa Marcus Thuram alihitaji dakika moja pekee kuwaweka uongozini vijana wa kocha Simeone Inzaghi baada ya pasi murwa kutoka kwa beki Denzil Dumfries ambaye aliongeza la pili dakika 20 badaye na kufanya mambo kuwa magoli 2-0

Hata hivyo Barcelona walikua na jambo lao wakipiga comeback ya haraka haraka kupitia winga matata tineja Lamine Yamal kunako dakika ya 24 kabla ya Ferran Torres kuweka mambo sawa dakika ya 38.

Hata hivyo licha ya kuchukua uongozi tena kupitia goli lake Denzel Dumfries dakika ya 63 The Catalans walihitaji dakika moja kusawazisha kupitia goli la kujifunga la kipa Yan Sommer baada ya mkwaju kali ilitumwa kimyani na winga wa Brazil Raphinha kunako dakika ya 64.

Mshambulizi Lamine Yamal akiwa na umri wa miaka 17 alikua anashiriki mechi yake ya 100 tangu anze kuchezea vinara hao wa Laliga.

Mechi ya mkondo wa pili itapigwa siku ya jumanne ugani San siro ambapo yeyote ana uwezo wa kupiga hatua kwenye nusu fainali hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version