News

Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta awataka vijana barani afrika kudumisha amani

Published

on

Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta ametoa wito kwa vijana katika bara hili la afrika kuwa katika mstari wa mbele katika kuhakikisha kwamba kuna umoja kwenye bara hili.

Kenyatta ambaye alikuwa akizungumza katika Kongamano la kila mwaka la viongozi wa vyama kwenye chuo kikuu cha Makere nchini Uganda amesema kuna umuhimu wa vijana kuchukua nafasi yao katika jamii na kuliongoza bara hili la Afrika.

Aidha, Kenyatta amesema vijana wana mchango mkubwa zaidi katika kuliimarisha bara hili na kusisitiza hoja ya kuondolewa kwa vikwazo vya kibiashara baina ya mataifa ya bara la Afrika ili kuimarisha sekta hiyo.

Picha kwa hisani | Rais mstaafu Uhuru Kenyatta akisalimiana na rais wa Uganda Yoweri Kaguta Mseveni

Vilevile, Kenyatta ametoa wito kwa wadau mbalimbali barani Afrika kuendelea kuangazia uvumbuzi kama njia mojawapo ya kuimarisha maisha ya vijana ili kuwaepusha na vishawishi ambavyo vinaweza kuwafanya kupotoka kimaadili.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version