News

Fedha za Shule Kusambazwa kwa Wakati, Asema Migos

Published

on

Waziri wa Elimu nchini Julius Migos amesema serikali imeweka mikakati muafaka ya kuhakikisha fedha za kusimamia shughuli za masomo zinasambazwa kwa wakati unaofaa shuleni.

Waziri Migos akisema tayari Wizara yake imefanya kikao na Wizara ya Fedha nchini kuhakikisha suala hilo linatekelezwa kikamilifu.

Aidha amesema hatua hiyo ni muhimu kwani itahakikisha wanafunzi wanapata huduma bora za masomo na kwamba itawawezesha walimu wakuu kusimamia shughuli za masomo bila changamoto.

Akizungumza mjini Mombasa baada ya kufungua rasmi kongamano la walimu wakuu wa shule za upili za kitaifa na shule za kufunza watoto wenye mahitaji maalum, Waziri Migos amesema hatua hiyo itasaidia kuboresha mazingira ya masomo.

Wakati huo huo amewahakikishia walimu wakuu kwamba ushirikiano kati ya Wizara ya Elimu na wadau wa sekta ya elimu nchini utahakikisha masuala ya elimu yanaendeshwa vyema. 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version