News

Wakaazi wa Matano Mane Walalamikia Ubovu wa Barabara

Published

on

Wakaazi wa maeneo ya Matano Mane katika wadi ya Sokoke kaunti ya Kilifi wameandamana na kufunga barabara ya kutoka Chuo cha ufundi cha Godoma inayopitia shule ya upili ya Vitengeni Baptist hadi Vitengeni Mjini wakilalamikia ubovu wa barabara hiyo.

Wakaazi hao wakiongozwa na Dan Mwangome, wamesema barabara hiyo imesalia kwa muda mrefu bila ya kukarabatiwa hali ambayo inatatiza shughuli za kibiashara na uchukuzi wa umma.

Wakaazi hao sasa wanasema mvua inazoendelea kuonyesha imesababisha shughuli za uchukuzi kukatizwa mara kwa mara huku viongozi wa eneo hilo wakishindwa kuwajibikia majukumu yao.

Wakati huo huo wakaazi hao wamemkosa Wanakandarasi aliyepewa zabuni ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kuzembea kuwajibikia majukumu yake ya kujenga barabara hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version