National News

Usalama Waimarishwa Mombasa Mfungo wa Ramadhan

Published

on

Kamishna wa kaunti ya Mombasa Mohammed Noor amewahakikishia waumini wa dini ya kiislamu na wakaazi wa kaunti ya Mombasa usalama wa kutosha wakati huu wa mfungo wa Ramadhan.

Noor amesema idara ya usalama katika kaunti hiyo imeongeza idadi ya maafisa wa usalama ambao wanashika doria nyakati za usiku hususan katika maeneo ya Likoni na Kisauni yanayotambulika zaidi kwa visa vya utovu wa usalama.

Aidha amewataka wakaazi kushirikiana na maafisa wa usalama katika kutoa taarifa za usalama.

Kwa upande wake Gavana wa Mombasa Abdulswamad Sharif Nassir amesema serikali ya kaunti hiyo imeweka taa za mtaani maarufu Street lights ili kuhakikisha usalama unaimarishwa.

Kauli za wawili hao zinajiri baada ya kushuhudiwa ongezeko la magenge ya kihalifu yanayowahangaisha wakaazi nyakati za usiku na alfajiri.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version