News

Oscar Nzai Apongeza Ushirikiano wa Utendakazi Kati ya Ruto na Raila Odinga

Published

on

Mwanasiasa Oscar Nzai amepongeza ushirikiano wa utendakazi kati ya Rais William Ruto na Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga, akisema ushirikiano huo utazikabili changamoto zinazowakumba wakenya.

Nzai amesema wakenya walikuwa wakilalamika kwamba wanapitia gharama ya juu ya maisha na kumshinikiza Odinga kutatua swala hilo kama mtetezi wao lakini utetezi huo hauezifanyika kama Odinga atakuwa nje ya serikali.

Katika kikao na Wanahabari, Nzai amesema njia pekee ya Odinga kuwaokoa wakenya kutokana changamoto mbalimbali nchini, ni kupitia ushirikiano wa utendakazi na Rais Ruto huku akiwarai wananchi kuwa na subra.

“Watu wanasema kwamba Raia amekuwa akiwatetea akiwa nje lakini kuna umuhimu wa Raila kuwa ndani ya serikali iliwatetee kutoka ndani kwa sababu kwamba tunalia sisi tunasema SHA ina matatizo na tunategemea kwamba Raila ndio mtetezi wetu kwa hivyo hapo nakuna dhambi kuna manufaa makubwa zaidi”, alisema Nzai.

Wakati uo huo Mwanasiasa huyo amewaria viongozi wanaohusika na mpango wa bima ya afya ya SHA kuhakikisha wanarekebisha changamoto zinazoshuhudiwa katika bima hiyo ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version