National News

Wanaharakati Kilifi Waishinikiza Serikali ya Kitaifa Kumaliza Ujenzi wa Daraja la Baricho

Published

on

Wanaharakati wa kijamii katika kaunti ya Kilifi wameishinikiza serikali ya kitaifa kukamilisha mradi wa ujenzi wa daraja la Baricho katika gatuzi dogo la Magarini ili kuboresha shughuli za uchukuzi na biashara.

Wakiongozwa na Kenza Ondieki, Wanaharakati hao wamesema ujenzi wa daraja hilo umechukua muda mrefu huku wenyeji wa eneo hilo wakiendelea kuathirika kiusafiri.

Ondiek amedokeza kwamba kukamilika kwa daraja hilo kutarahisisha usafirishaji wa bidhaa za kilimo hadi sokoni sawa na kuimarisha uchumi wa eneo hilo.

Kwa upande wake Mbunge wa zamani wa Magarini Joseph Kasena Yeri amekariri kwamba kukamilika kwa ujenzi wa daraja hilo kutasaidia wakaazi wengi wa Magarini wanaotafuta huduma muhimu mjini Malindi kuzipata kwa urahisi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version