News

Boresheni Vyuo vya Kiufundi, Jacinta Fondo

Published

on

Serikali ya kaunti ya Kilifi imehimizwa kuboresha vyuo vya kiufundi vya TVET ili kuviwezesha kutoa mafunzo ya hadhi ya juu kwa wanafunzi.

Kulingana na Kiongozi wa vijana katika kaunti ya Kilifi Jacinta Fondo, imekuwa ngumu kwa vijana wanaofuzu kwenye vyuo vya kiufundi vya kaunti ya Kilifi kupata kazi kutokana na ukosefu wa ufahamu wa baadhi ya matumizi wa vifaa vya kisasa.

Jacinta amesema kampuni nyingi huenda zikakosa kuwaajiri vijana wanaotoka kwenye vyuo vya TVETs vya Kilifii kwani hawana uzoefu wa kutumia vifaa vya kisasa.

Wakati huo huo amependekeza serikali ya kaunti ya Kilifi kubuni ajira kwa vijana ili wanapofuzu wasitaabike kutafuta kazi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version